MKE au MUME ana haki ya kumshtaki na kumdai fidia mtu ambaye anamshawishi mwenza wake kwa lengo la kuvunja ndoa yao.
KIFUNGU cha 73 cha sheria ya ndoa ya mwaka 1971 na marekebisho yake kinasema;
MUME au MKE ana haki ya kumshtaki mtu mwingine yeyote ambaye anamshawishi/kumtongoza mwanandoa wake kwa lengo la kuvunja ndoa yao na kuwatenganisha.
Shauri la aina hii litakataliwa na kufutwa na mahakama kama itabainika wazi kuwa tabia za mwanandoa anayedai fidia zilimpelekea mwenza wake kujihusisha kimapenzi na MTU mwingine.
Jungu la sheria Tanzania ✔️
#sherianatehama

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿