Baada ya wazazi kutengana, mtoto ana haki ya kuendelea kupata matunzo kutoka kwa wazazi pamoja na kuendelea kupata elimu ya kiwango kilekile alichokuwa akipata mtoto kabla ya kutengana kwa wazazi wake.
Mtoto pia ana haki ya kuishi na mzazi ambaye kwa maoni ya mahakama, anaweza kumlea na kukidhi mahitaji ya mtoto bila kuathiri ukuaji wake kama mtoto.
Mtoto ana haki ya kumtembelea na kukaa na mzazi mwingine wakati wowote anapojiskia isipokuwa tu kama kufanya hivyo kunaathiri ratiba yake ya shule.
Ni mtazamo wa kisheria kwamba mtoto wa chini ya miaka saba atakaa na mama yake mzazi lakini mahakama kuzingatia sababu zingine inaweza kuagiza kinyume chake.
Jungu la sheria Tanzania ✔️.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿