SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI SURA YA 20 ILIYOREJEWA MWAKA 2019.
KIFUNGU CHA 222 KINASEMA,
Iwapo, katika kesi yoyote ambayo mahakama ya chini ina mamlaka kusikiliza na kuamua, mtuhumiwa amehudhuria kwa kutii wito aliopelekewa katika muda na mahali palipoteuliwa katika wito kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi, au ameletwa mbele ya mahakama akiwa amekamatwa, kwa hiyo, kama mlalamikaji, baada ya kupewa taarifa ya muda na mahali palipoteuliwa kwa ajili ya kusikiliza shitaka hatahudhuria, mahakama italazimika kutupilia mbali shitaka na kumwachia huru mtuhumiwa, isipokuwa kama kwa sababu fulani, italazimika kufikiri ni vema kuahirisha usikilizaji, wa kesi mpaka tarehe nyingine na, wakati akisubiri usikilizaji ulioahirishwa, ama kumuachia mtuhumiwa kwa dhamana au kumweka rumande au kuchukua dhamana kwa ajili ya kuhudhuria kwake kama mahakama itakavyoona inafaa.
Imeandikwa na Mwanasheria
Johnson Yesaya Mgelwa
Wa Jungu la sheria Tanzania
0758218269/0628729934
0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿