SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI SURA YA 20 ILIYOREJEWA MWAKA 2019.
KIFUNGU CHA 187 KINASEMA;
Hakuna mtoto atakayeruhusiwa kuwa mahakamani wakati wa shauri la mtu yoyote mwingine anayeshitakiwa kwa kosa au wakati wa mwenendo wa mwanzo wa shauri hilo isipokuwa katika muda huo ambapo uwepo wake utahitajika kama shahidi au vinginevyo kwa madhumuni ya haki; na mtoto yeyote aliye mahakamani wakati chini ya kifungu hiki haruhusiwi kuwepo ataamuriwa kuondolewa; lakini hiki kifungu hakitatumika kwa wahudumu, maafisa sheria, makarani au watu wengine wanaotakiwa kuhudhuria mahakamani kwa madhumuni yanayohusiana na ajira zao.
Imeandikwa na
Mwanasheria,
Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm)
Wa Jungu la sheria Tanzania
0758218269/0628729934
0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿