Ticker

6/recent/ticker-posts

Kudharau Mahakama Kosa la Jinai.



Kudharau Mahakama kosa la Jinai ⚖️

Kwa mujibu wa Kifungu cha 114 cha Kanuni ya Adhabu, mtu yeyote anayefanya jambo lolote linalodharau au kuharibu heshima ya Mahakama au kuathiri mwenendo wa kesi, anakuwa ametenda kosa la kudharau mahakama.

🚫 Vitendo vinavyohesabika kama Kudharau Mahakama ni pamoja na:

🔹 Kuonyesha dharau kwa maneno au matendo ndani ya ukumbi wa Mahakama.

🔹 Kukataa kuapa au kutoa ushahidi baada ya kuitwa kama shahidi.

🔹 Kusababisha fujo au kero wakati wa mwenendo wa kesi.

🔹 Kuchapisha au kusema habari zinazopotosha au zinazoathiri mwelekeo wa kesi.

🔹 Kuchapisha ushahidi wa kesi ya faragha.

🔹 Kuingilia au kushawishi shahidi kutoa ushahidi kwa njia isiyo halali.

🔹 Kumfuta kazi mfanyakazi kwa sababu ya kutoa ushahidi mahakamani.

🔹 Kuchukua tena mali au mtoto ambaye Mahakama imetoa uamuzi kuhusu umiliki au uangalizi wake.

🔹 Kukataa kulipa fidia au gharama kama ilivyoamuliwa na Mahakama.

🔹 Kufanya tendo lolote la makusudi la kudharau Mahakama au mwenendo wa kesi.

⚖️ Adhabu:

Kifungo cha hadi miezi sita au faini isiyozidi shilingi 100,000.

👉 Ikiwa kosa limefanyika mbele ya Mahakama, jaji au hakimu anaweza kumhukumu mhalifu siku hiyo hiyo kwa faini ya shilingi 400 au kifungo cha hadi miezi sita.

🔍 NB: Hii ni tofauti na mamlaka ya Mahakama Kuu katika kushughulikia makosa ya dharau.

#SheriaZaTanzania #ContemptOfCourt #HeshimaKwaMahakama #JunguLaSheria ⚖️

     ⚖️ Tatizo Lako la Kisheria Linahitaji Majibu Sahihi?

Elimu ya sheria inayotolewa kwenye makala hii ni ya jumla. Ikiwa unahitaji ufafanuzi kuhusu hali yako binafsi, unaweza kuongea moja kwa moja na Mwanasheria na kupata ushauri unaoendana na mazingira yako.

✅ Utakachopata

✔️ Uchambuzi wa suala lako la kisheria

✔️ Majibu ya maswali yako moja kwa moja

✔️ Mwongozo wa hatua za kuchukua

✔️ Ushauri wa kitaalamu unaozingatia mazingira yako

✔️ Usiri wa kitaalamu katika mawasiliano yote

📚 Maeneo Tunayotoa Ushauri

Ardhi • Mirathi • Ndoa na Talaka • Ajira • Mikataba • Madeni • Biashara • Mashauri ya Madai • Mashauri ya Jinai na masuala mengine ya kisheria.

💰 Ada ya Ushauri: TSh 30,000 Tu

📲 Fanya Malipo Kupitia Mojawapo ya Njia Zifuatazo

✅ Airtel Money LIPA: 13970429

✅ Yas/Tigo LIPA: 18401500

✅ M-Pesa Wakala: 826910

✅ Selcom Lipa: 61122934

✅ CRDB Lipa TANQR: 11692089


Jina la Mpokeaji:
Johnson Yesaya Mgelwa

📩 Baada ya Kufanya Malipo

Tuma ujumbe mfupi wa kuthibitisha malipo yako kupitia WhatsApp au SMS. Utapigiwa simu ndani ya dakika 10 kwa ushauri wa kisheria.

💬 TUMA UTHIBITISHO WA MALIPO

+255 628 729 934

Usifanye Maamuzi ya Kisheria Bila Ushauri wa Kitaalamu.

Chapisha Maoni

0 Maoni