IBARA ya 18 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari za dhana zozote
kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana Uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
Jungu la sheria Tanzania ✔️
#sheria
#katiba

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿