Ticker

6/recent/ticker-posts

MDAIWA ANAPASWA KULIPWA POSHO NA MDAI ANAPOWEKWA KIZUIZINI KUTOKANA NA MAOMBI YA MDAI



MDAIWA ANAPASWA KULIPWA POSHO NA MDAI ANAPOWEKWA KIZUIZINI KUTOKANA NA MAOMBI YA MDAI



Kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Kesi/Mashauri ya Madai, SURA 33 kanuni ya XXI (28, 29, 35 na 38).


Kuna namna nyingi zinazotumika kutekeleza hukumu katika mashauri ya madai. Kukamata na kuuza Mali za mdaiwa ni namna moja, lakini kumuweke kizuizini mdaiwa katika kesi ya madai pia ni namna nyingine inaposhindikana namna ya kwanza hapo juu.


Maelezo yetu yatajikita zaidi katika namna ya pili, kuhusu kumuweka kizuizini mdaiwa wa madai.


Baada ya mahakama kuamua kuwa mdaiwa anatakiwa kulipa kiasi fulani cha fedha kama hukumu, au fidia kwa mdai, mdai anaweza kuiomba mahakama kutoa amri ya kukamata na kuuza mali za mdaiwa, lakini endapo itashindikana kwasababu za mdaiwa kutokuwa na mali yeyote.


Mdai anaweza kuiomba mahakama kukamatwa na kuwekwa kizuizini mdaiwa ambaye ameshindwa kulipa kiwango cha fedha kama hukumu au fidia kwa mdai.


Mahakama ikijiridhisha, na kupanga kiwango cha posho ambacho atalipwa mdaiwa muda wote akiwa kizuizini, Basi mahakama itatoa amri ya kuwekwa kizuizini kwa mdaiwa (mfungwa wa madai) ambapo muda wa kukaa kizuizini haupaswi kuzidi miezi sita.


Mdai atawajibika kumhudumia mdaiwa, na kumlipa posho kila mwezi na mengineyo kama itakavyoamuriwa na mahakama.


Jungu la sheria Tanzania.

     ⚖️ Tatizo Lako la Kisheria Linahitaji Majibu Sahihi?

Elimu ya sheria inayotolewa kwenye makala hii ni ya jumla. Ikiwa unahitaji ufafanuzi kuhusu hali yako binafsi, unaweza kuongea moja kwa moja na Mwanasheria na kupata ushauri unaoendana na mazingira yako.

✅ Utakachopata

✔️ Uchambuzi wa suala lako la kisheria

✔️ Majibu ya maswali yako moja kwa moja

✔️ Mwongozo wa hatua za kuchukua

✔️ Ushauri wa kitaalamu unaozingatia mazingira yako

✔️ Usiri wa kitaalamu katika mawasiliano yote

📚 Maeneo Tunayotoa Ushauri

Ardhi • Mirathi • Ndoa na Talaka • Ajira • Mikataba • Madeni • Biashara • Mashauri ya Madai • Mashauri ya Jinai na masuala mengine ya kisheria.

💰 Ada ya Ushauri: TSh 30,000 Tu

📲 Fanya Malipo Kupitia Mojawapo ya Njia Zifuatazo

✅ Airtel Money LIPA: 13970429

✅ Yas/Tigo LIPA: 18401500

✅ M-Pesa Wakala: 826910

✅ Selcom Lipa: 61122934

✅ CRDB Lipa TANQR: 11692089


Jina la Mpokeaji:
Johnson Yesaya Mgelwa

📩 Baada ya Kufanya Malipo

Tuma ujumbe mfupi wa kuthibitisha malipo yako kupitia WhatsApp au SMS. Utapigiwa simu ndani ya dakika 10 kwa ushauri wa kisheria.

💬 TUMA UTHIBITISHO WA MALIPO

+255 628 729 934

Usifanye Maamuzi ya Kisheria Bila Ushauri wa Kitaalamu.

Chapisha Maoni

0 Maoni