Ticker

6/recent/ticker-posts

KUWATUMIA WATOTO KINGONO NI KOSA LA JINAI.


 KUWATUMIA WATOTO KINGONO NI KOSA LA JINAI.

KANUNI YA ADHABU SURA YA 16 KIFUNGU 138B.

Kifungu tajwa hapo juu kinasema;

138B.-(1) Mtu yeyote ambaye- 

(a) akiwa anafahamu anamruhusu mtoto yeyote kuwa kwenye sehemu yoyote kwa nia ya kumsababisha mtoto kudhalilishwa kijinsia au kushiriki kwa namna yoyote katika matendo ya ngono au maonyesho ya ngono;

(b) anajifanya kuwa ni kuwadi wa mtoto kwa nia ya kufanya ngono au namna yoyote ya udhalilishaji kwa ngono, au maonyesho ya ngono;

(c) anamlaghai mtu kuwa yeye ni mteja wa mtoto kwa nia ya ngono au aina yeyote ya udhalilishaji wa kijinsia, au maonyesho ya ngono, kwa njia ya matangazo au kwa kutumia vyombo vya habari, matangazo kwa njia ya mdomo au namna nyingine zinazofanana na hizo;

(d) anatumia vibaya uwezo wake au mahusiano yake aliyonayo kwa mtoto, akamlaghai mtoto kufanya matendo ya ngono au namna yoyote ya udhalilishaji wa kijinsia au maonyesho ya kudhalilisha ya ngono;

(e) anamtishia, au akitumia nguvu kwa mtoto, kwa nia ya kumlazimisha mtoto kufanya ngono au kwa namna yoyote ya kumdhalilisha mtoto kwa ngono au maonyesho ya ngono; 

(f) anampa mtoto au wazazi wake fedha, vitu au mafao mengine kwa nia ya kumkuwadia mtoto huyo afanye ngono au namna yoyote ya udhalilishaji wa ngono au maonyesho ya ngono,

Atatenda kosa la kumtumia mtoto kwenye matendo ya ngono na atawajibika kwa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka kumi na mitano jela na kisichozidi miaka thelathini.

     ⚖️ Tatizo Lako la Kisheria Linahitaji Majibu Sahihi?

Elimu ya sheria inayotolewa kwenye makala hii ni ya jumla. Ikiwa unahitaji ufafanuzi kuhusu hali yako binafsi, unaweza kuongea moja kwa moja na Mwanasheria na kupata ushauri unaoendana na mazingira yako.

✅ Utakachopata

✔️ Uchambuzi wa suala lako la kisheria

✔️ Majibu ya maswali yako moja kwa moja

✔️ Mwongozo wa hatua za kuchukua

✔️ Ushauri wa kitaalamu unaozingatia mazingira yako

✔️ Usiri wa kitaalamu katika mawasiliano yote

📚 Maeneo Tunayotoa Ushauri

Ardhi • Mirathi • Ndoa na Talaka • Ajira • Mikataba • Madeni • Biashara • Mashauri ya Madai • Mashauri ya Jinai na masuala mengine ya kisheria.

💰 Ada ya Ushauri: TSh 30,000 Tu

📲 Fanya Malipo Kupitia Mojawapo ya Njia Zifuatazo

✅ Airtel Money LIPA: 13970429

✅ Yas/Tigo LIPA: 18401500

✅ M-Pesa Wakala: 826910

✅ Selcom Lipa: 61122934

✅ CRDB Lipa TANQR: 11692089


Jina la Mpokeaji:
Johnson Yesaya Mgelwa

📩 Baada ya Kufanya Malipo

Tuma ujumbe mfupi wa kuthibitisha malipo yako kupitia WhatsApp au SMS. Utapigiwa simu ndani ya dakika 10 kwa ushauri wa kisheria.

💬 TUMA UTHIBITISHO WA MALIPO

+255 628 729 934

Usifanye Maamuzi ya Kisheria Bila Ushauri wa Kitaalamu.

Chapisha Maoni

0 Maoni